Search This Blog

Thursday, November 3, 2022

USHUHUDA WA KWELI NAMBA 92

    




 Hebu nisimulie hiki kisa changu...



Jumanne 23-08-2019.



Ilikuwa saa nne na nusu usiku nikiwa nimeketi sebuleni,mara gafula mzee akatoka chumbani na kuanza kunitukana matusi ya nguoni...

"Kijana gani wewe kazi kula na kujaza choo,huoni wenzio wanafanya kazi na wanategemewa na wazazi wao...ni bora ningezaa hata mbuzi ningefaidi mchuzi.."

Mara ghafula nashutuka kofi hili hapa sijakaa vizuri ngumi hii hapa,nikasimama imara na kumkazia tu macho...wadogo zangu na mama yangu wakitazama tu pasi na kusema neno.

Nikageuka taratibu na kutoka nje,chozi la uchungu likanitoka ilikuwa ni siku mbili tu toka nifukuzwe shule moja niliyokwenda kuomba ajira ya kujitolea..ati hawawezi kuajiri kiziwi!.

Nilitazama anga jeusi lililosheheni nyota nyingi,mwezi uliotoa nuru angavu nikajiuliza "Mungu upo wapi?".. Nikaingia chumbani na kuvaa viatu.. Nikatoka naenda wapi? Sijui!

Nikaambaa nisijue kama nakanyaga ardhi au ninapaa,napishana na mtu ama kisiki,ilinichukua nusu saa kuuacha mtaa wetu nikaingia mtaa wa pili,huu ulikuwa na watu wachache zaidi na nyumba zilikuwa mbalimbali kiasi.

Nikakatiza pembeni ya makaburi,nikasimama,nikayatazama na kujiuliza " kwanini nisingekuwa nimelala pale? Nipumzike!"...loooh lakini sauti nyingine ikaniambia "una uhakika ukilala pale utapumzika? Nikagutuka nikatazama huku na huko hakuna kiumbe nikaongoza njia kuliacha eneo la makaburi na kuzidi kupotelea mbali zaidi na nyumbani.



Hatimaye nikawasili sehemu pweke,barabara kubwa ya kokoto,kulia na kushoto kukiwa na msitu na vichaka vingi,kiza ni kingi kutupia macho simu yangu ni saa sita na robo usiku!

Ikafika mahali kuna njia panda na upande wa kulia kuna mti mkubwa sana aina ya mbuyu mahali pana pana joto sana bwana,pana joto kali,mapigo ya moyo yakanienda mbio " duuucha dunduncha ducha dunduncha" sasa mapigo niliyasikia hadi masikioni..

Nywele zikanisimama na vipele vya uoga vikanitoka hewa ikawa nzito na uvumilivu ukaniisha na sasa nikatimua mbio hata nilipoliacha eneo lile kwa umbali wa mita mia mbili hivi,na sasa nikaanza kutoka katika makazi ya watu.

Kufika hapa ikanipasa kujiuliza ni wapi naelekea,sikuwa napajua napoelekea kumbukumbu ya misukosuko ya kimaisha na masimango yasiyoisha zikanijia,woga wote ukabiisha donge zito la uchungu,hasira na kukata tamaa likanivaa,machozi yakanitoka,nikashika njia na kuendelea na safari,safari isiyojulikana!

Baada ya mwendo wa dakika ishirini hivi nikaingia katika barabara kubwa ya lami,nikashika uelekeo wa kushoto,ilielekea ufukweni,baada ya masaa mawili hatimaye nikawasili ufukweni,nikazitupia macho hoteli kadhaa zilizotamalaki eneo lile,nikaachana nazo na kushuka mchangani mbali kidogi na mahoteli yale,nikajikalisha kitako na kutafakari nilipotoka,nilupo na ninapoelekea,lakini mbona mbele kyna kiza kizito!





KIZAAZAA!

Hatimaye saa tisa ikawadia,nilichoka,na sasa ilikuwa ni safari ya kurudi,nikajizoa zoa na kushika njia kurudi nyumbani,bahati nzuri barabara hii ilikuwa na taa hivyo ikawa ahueni kwangu.

Baada ya mwendo wa dakika arobaini hivi nikahisi kama kwamba kulikuwa na mtu nyuma yangu,nikageuka kwa kasi, ebo! Nikaona nguo ya rangi ya khaki,aidha gauni au kanzu ikiishia na kufutika machoni kwangu....

Mshtuko uluonipata ukanifanya hata nguvu za miguu ziniishie nikajikuta nikiketi katika mfereji mfupi uliojengwa pembeni ya barabara.

"Ni nini hiki? Ni kweli au ni mawazo yangu tu?" Nikajiuliza,nukatazama huku na huko hali ni shwari,labda niliangalia vibaya bwana nikajizoazoa na kuendelea na safari..

Kiroja kingine tena! Ati nina vivuli viwili,kimoja ni changu na kimoja kimevaa kanzu kama si gauni!(mataa ya barabarani yanawaka hivyo mtu akipita kivuli chake kinaonekana kwa ufasaha kabisa) nikatetemeka kwa woga,nikageuka nyuma ati nacho kikageuka! Nikawa natembea kwa kurudi kinyume nyume,ati nacho kinarudi kinyume nyume!.



Lakini mbona kivuli changu kupo mbele yangu hiki cha nyuma ni cha nani? Na tumeachana umbali wa hatua kama tatu hivi toka kilipo hadi nilipo,nikaona huu sasa utani,nikifa si nife tu ebo! Nikakata shauri kukifuata he! Ati nacho kinageuza kila nikikifuata nacho kinaenda nyuma zaidi,ikabidi nikikimbize sasa..kikapotea.

Nikageuka na kuanza kukimbia kwa taratibu mithiri ya mbio za riadha,nikachoka nikaanza kutembea baada ya mwemdo mrefu kivuli kile kikarudi! Sikusimama nikaendelea kutembea tu.

Hata hivyo nikaanza kuhisi mwili kuchoka sana,miguu inauma na usingizi ni mwingi sana,nikajikalisha juu ya ukingo wa karavati kutafuta pumzi maana ilikuwa ni safari ya masaa mawili zaidi hadi nifike nyumbani...nikaanza kusinzia na hatinaye fahamu zikakomea hapo.

Kelele za watoto wakicheza ndizo zilizonigutusha,nikafumbua macho..afanalek! Nilikuwa nimelala chumbani kwangu..miguu ilikuwa imevimba kiasi na mwili mzima ulikuwa unaniuma...



"Lakini mimi mbona nilikuwa kule barabarani?" Nikajiuliza nisijue kilichotokea,nikaamka na kulibinua bati ninalotumia kama mlango,nikapenyeza kiubavuubavu hadi nje.

Nikawatazama nyusoni niliowakuta nje,wapo kawaida,hawana hata habari,pengine niliokotwa na wasamaria wema! Lakini mbona watu wapo kawaida kama hakuna kitu?...nikashindwa kuvumilia nikaamua kumuuliza mama ni muda gani niliingia kulala!

Akanijibu "we si uliingia kulala saa nne weww? Maswali gani hayo usinisumbue" ni nani aloyenirudisha nyumbani,na kile kivuli ni kiumbe gani? Je ndicho kilichonirudisha nyumbani? Lakini hakijanidhuru, hili ni fumbo niishilo nalo hata sasa kuna wakati natamani kukiona tena kivuli kile kilichovalia kanzu au gauni lililopauka lakini hakitokei tena.





USHUHUDA WA KWELI NAMBA 91

   




 Binafsi sijawahi kutana na hayo mauzauza, na ninaomba MUNGU nisikutane nayo maana nitakufa hapo hapo. Ila kuna visa viwili nilihadithiwa na wazee wangu.

Cha kwanza ni baba yangu mzazi, wakati akiwa kijana barobaro alikuwa anapenda sana kutembea usiku. Alikuwa anaishi maeneo ya Tegeta. Siku moja wakati anarudi usiku akiwa anatembea akawa anasikia kama kuna mtu nyuma yake anamfuata ila akigeuka hamuoni, akakaza mpaka akafika magetoni. Akajiandaa kulala akafunga mlango na kuzima taa akapanda kitandani.

Wakati bado usingizi haujampitia vizuri akawa anahisi kama mtu anafungua mlango kwa nje anamchungulia, akapotezea akalala. Katikati ya usingizi akahisi kukabwa na mtu akiwa amelala, akajitahidi kujitetea lakini bado, akajaribu kupapasa akahisi ameshika jitu lenye manyoya mengi sana mikononi kama manyani yale. Hapo ndo akajua shit just got real. Akaamka akawasha taa hakulala mpaka asubuhi. Alikuja kusaidiwa na mzee mmoja hv alikuwa anakaa mwenge almaarufu kama Babu wa Mwenge marehemu. Akamwambia lilikuwa jini alikumbana nalo njiani. Lakini bado since then hakukoma kutembea usiku.



Cha pili ni mama yangu. Ni mchaga wa rombo, anakwambia zamani walipokuwa mabinti wadogo kulikuwa na majitu yanaitwa "Mangauneri" wajuzi mtanisaidia. Walikuwa kama binadamu tu wanakuja hadi nyumbani mnakula nao chakula cha usiku ila wanakijiji walikuwa wanayajua kwa hiyo wanamkaribisha tu akimaliza chakula anaaga anaondoka. Sasa baada ya hapo ni kuwasha moto mkubwa maana akiondoka anasikilizia mkishalala anakuja anachukua vijinga anawachoma navyo especially matakoni. Waliokuwa wanapasua mbao porini walikuwa wanakutana nao sana.





Wednesday, November 2, 2022

USHUHUDA WA KWELI NAMBA 25.

   




ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.



Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.



Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.



Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.



Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.



lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama



USHUHUDA WA KWELI NAMBA 90

  




 Wacha na Mimi niwape mkasa niliyoshuhudia katika mahakama moja miongoni mwa wilaya za Tanga.

Nikiwa katika harakati za kutekeleza majukumu ya kikazi nilipanga nyumba moja hivi iko vizuri tu.wapangaji tulikuwa watatu tu, baba mwenye nyumba Ni kijana mwenzetu ana mishe zake. Sasa bhana huyu baba mwenye nyumba kwenye biashara zake akafanya magumashi yaliyompelekea kushatakiwa na kufunguliwa kesi mahakamani. Kesi ilikuwa kubwa ya kumfunga kifungo kirefu tu. Kwa kuwa huyu baba mwenye nyumba tulikuwa tukielewana stori kwa Sana akanambia nimsindikize mahali kwa mganga. Tukaenda aisee tulipofika mganga akatueleza shida tuliyoendea kesi jinsi ilivyo na imebaki shahidi tu kuja kutoa ushahidi siku ya kesi jamaa ahukumiwe kwa namna yoyote jamaa hachomoki. Mganga akasema kanileteeni Nazi moja tu na si kitu kingine duh tukasema hapa hamna mganga. Tukaenda nunua Nazi tukampelekea, mganga akaandika maneno ya kiarabu kwenye ile Nazi kwa juu ikiwa haijapasuliwa ( maandishi yalikuwa ya rangi nyekundu). Kisha akasema saa 8 usiku ile Nazi ikapasuliwe njia panda ya kuelekea mahakamani.

Tuliporudi home tukawa tunasema mganga mzinguwaji kesi kubwa yy anatufanyia mzaha, basi saa nane usiku tukaenda njia panda ya kuelekea mahakamani jamaa jamaa akajifunga kaniki nyeusi Kisha akaipasua kama alivyoelekeza mganga.

Siku ya kesi ikafika ndipo nilipojuwa kuwa dunia no Zaidi ya tunavyoiona. Jamaa kafikishwa kizimbani kasomewa mashtaka kakataa akaitwa shahidi wa Kwanza, hakimu Kila swali akimuuliza shahidi anasema kasahau hakumbuki kitu, shahidi wa pili ndiye was muhimu Sana aisee jamaa alivyopanda kutoa ushahidi alikuwa bubu seriousky kudadeki acheni tu Kila akiulizwa anashindwa kuongea anabaki baaaa...baaaa...mmmm. Hakimu alidata akaahurisha kesi.

Siku tajwa ya kesi kufika hakuna shihidi alokuja Tena na Tena. Hakimu akafuta kesi na jamaa akawa huru.

Hivi vitu vipo aisee Ni mpaka ushuhudie ndiyo utaamini.




USHUHUDA WA KWELI NAMBA 89

  



 ..Arusha..

Mimi nilikuwa nikiumwa nikienda shule tu na ilikuwa shule ya msingi..nikiruhusiwa kwenda nyumbani nakuwa mzima wa afya.Ikawa hivyohivyo..



Kuna kipindi ghafla uwezo wa kuona ukawa unapungua yaani nlikuwa nikiangalia mbele naona kama ukungu tu...ilikuwa balaaa.ila kuna mtu alinipa dawa ya majani .nikapona



Kuna siku niliumwa ..mpaka watu walijua nimekufa wakaanza kulia plus maandalizi ya kunizimisha macho nk.na hapo anae nizimisha macho ni bibi mmoja ambae alikuwa mchawi balaa.lakini MUNGU alikuwa mwema kwangu.nilizinduka ila jicho moja likawa limepata kengeza ..

Na mwanzo nilikuwa mzima kabisa nilikuwa na macho ya kawaida kabisa



Lakini tokea siku hiyo sijawahi kumwa tena na sasa ni mtu mzima na maisha yangu..

Na sijui sababu ya mm kuumwa ilikuwa nn

..uchawi upo tusali sana na kuomba





USHUHUDA WA KWELI NAMBA 88

  






 Mimi nilikuwa siamini hizo mambo lakn kipind cha wife ana ujauzito wa mtt wetu wa kwanza.. nikiwa mchanga kbsa kiimani,siku hio nakumbuka tumelala tukaota ndoto moja mm na wife.. ndoto ilikuwa ni mmama mmoja anasema anataka mtt alieko tumboni ili amtoe kafara,tukashtuka.. baada ya kushtuka tukasikia mipaka inalia nyuma ya nyumba kwa sauti kubwa,nilikuwa nmeshafundishwa kuomba na kukemea.. asee niliomba sana usiku huo kwa ujasiri na nguvu maana wife yeye muda huo alikuwa analalamika tumbo linamuuma na mtt alikuwa anarukaruka hatar tumboni... wakat naendelea kuomba kwa nguvu na ujasiri nkaanza kusikia sauti za paka zinaendelea kusogea mbali na nyumba lakn kitu ambacho kilikuja kunishangaza mpka sasa ni kwamba wakat naendelea kuomba nilianza kusikia vishindo kbsa kwnye bati na nyumba haikuwa na celingboard yaan vile vishindo ni kama mtu akiwa anatembea juu ya bati ikatembea alafu nkasikia hiko kishindo kimetua kama kudondoka nyuma ya chumba changu... nkapata ujasiri wa kukatisha maombi ghafla nkafungua mlango kwenda kuangalia nione hata nyayo.. bt sikuona chochote... Hata siku wife kaumwa na uchungu mida ya jioni mapaka yalilia sana siku hio.. akaenda hosptal akajifungua na alijifungulia pale amana enzi hizo na wakt anajifungua paka alitokea akabeba na kondo lake la nyuma,akatoka salama... tukaendelea kumlea mtt wetu lakn mtt alikuwa anaumwa kila siku mwisho hasa kuharisha na kutapika na tukienda hosptal ugonjwa hauonekani..so mtt alipofika mwaka na miez miwil sku hio hali ya mtt ikiwa dhoofu wazaz wakaomba tupeleke mtt akaugulie huko.. basi nkamwambia wife akapaki akapanda daladala kwenda home.. akiwa kwnye daladala mzee mmoja mwnye mapetepete mengi ya rangirangi na kanzu na kibalaghashia chake akauliza huyu mtt anaonekana anaumwa eeh wife akamjibu ndio.. akamwambia ugonjwa wake sio wa hosptalin bt hakumwelewa alimaanisha nn,kufika home kakaa siku ya kwnza siku ya pili usiku akiwa amelala akaota ndoto wamekuja mmama na kundi lake kavaa kaniki akasema mmalizieni kabiss huyo mtoto afu ndoto ikakatika...kesho yake asbh mie nko mtaani napiga mzgo wife akanipgia simu hali ya mtt imechange na kwl haikupita dk kumi wife akiwa anamnyonyesha mtt akamfia hapohapo... R.I.P katt kangu ka kike first born wangu..




BLOG