Search This Blog

Wednesday, November 2, 2022

USHUHUDA WA KWELI NAMBA 12

  









Miaka ya nyuma tunatoka mererani usiku wa manane tuko na pikipiki almaarufu baja tullikutakana na moto mkubwa ukiwa umetanda barabarani kama vile unavuka ,tulikuwa sita tukajishauri sana lakini kwasababu tulikuwa wengi tulipata ujasiri wa kupita ila cha kushangaza tulivuka na hatukuungua wala kuhisi chochote kuangalia nyuma baada ya kuvuka moto uko vile vile



Niliwahi kutongoza mtoto wa ustadh mmoja kama mchepuko , mzee wake akanistukia , akaniacha tu ,ila balaa kila nikienda kupiga ,kitu hakisimami hadi tunatoka ila nikienda sehemu zingine napiga kama kawaida



USHUHUDA WA KWELI NAMBA 11

  







Hii ilitokea Tanga wilaya M. Kuna mganga fulani alikua mganga akaona akatoe huduma za kiganga wilaya M akitokea wilaya K. Basi alifikia nyumba ya jamaa mmoja na kumueleza kwamba amekuja hapo kutoa huduma kama kuna mwenye tatizo lolote aje. Basi mganga akapewa chakula akala na kupewa mahali pa kulala. Muda kufika akaenda kulala na mikoba yake. Kulipokucha adibuhi mganga alijikuta yuko nyumbani kwake wilaya K na mke wake na mikoba yake



USHUHUDA WA KWELI NAMBA 10

  



Miaka 6 iliyopita Kuna rafiki alikwenda kijijini kwa Bibi yake kusalimia..alivyofika kijijini akatembea na Mume wa mtu...mke wa mwenye Mume akamlogezea ukimwi.



Rafiki alianza kuumwa ilibidi aletwe dar kwa vipimo zaidi ..kila akipimwa hakuna kitu na hali inazidi kuwa mbaya..na uumwaji wake ni ule ule wa wagonjwa wa ukimwi..hali ikazidi kuwa mbaya hadi kufikia kuwa mtu wa kitandani tu..Mama yake mdogo akajiongeza akamleta mtaalam akaweka kambi nyumbani kwao week mbili..week ya tatu rafiki mzima hakuwa na hata dalili Kama alitoka kuumwa ule ugonjwa...uchawi upo jamani.





USHUHUDA WA KWELI NAMBA 9

  






Kisa cha kwanza ambacho kinanivutia hadi leo ilikua mwaka 1998, Niko na jamaa yangu, Tunatokea Shule ya Wasichana Kifungilo tunarudi shuleni kwetu Magamba Secondary (now Sebastian Kolowa University)! Usafiri miaka ile usafiri ulikua wa shida sana, tukawa tunasubiri usafiri pale Lukozi, SAA Tisa au kumi hivi jioni. Mvua ikaanza kunyesha, wenyeji wakasema kuwa Mvua haitanyesha kwa kuwa Mzee Fulani yuko shambani kwake anauza mapeasi yake.



Ghafla yule Mzee akawa anapita, aiseee seriously kwa Mara ya kwanza tangu nizaliwe sijawahi kuona MTU hanyeshewi na mvua! Yaani mvua inanyesha lakini yeye hanyeshewi kabisa





USHUHUDA WA KWELI NAMBA 7

  




Yuko dogo mmoja alikua anasoma B sekondary. Alikua anamchukua mke wa mtu. Mtu mwenyewe alikua nje ya nchi kimasomo. Ndugu zake msomi hawakupendezewa shemeji Yao aliwe na student. Kuna siku dogo wakapanga na bibie wakapeane penzi kwenye minazi. Enzi hizo gesti wanaingia wenye pesa zao.



Dogo alikua dent hana pesa. Basi kweli muda kufika mke akafika na mechi ikaanza bila refa. Dogo akapakua mzigo kufika kileleni utamu Ulipozidi ni kawaida mtu kufunga macho. Basi dogo wakati anafyatua risasi alimkumbatia mke wa mtu kisawasawa huku amefunga macho. Ile kumaliza na kufumbua macho akajikuta alikua anafanya mapenzi na kisiki cha mnazi na sio mtu. Dogo kutoka pale hakurudi shuleni. Alipanda basi la Dar na kuacha shule. Sidhani kama alisharudi wilaya ya B.





USHUHUDA WA KWELI NAMBA 6

  




Nishawahi sikia kisa kinachohusishwa na uchawi



Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri



Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma



Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma



Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea



Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge



si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.



wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.



Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele



Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"





BLOG